Thursday, January 8, 2009

JIONEENI WENYEWE

VIVA LE TANZANIA mtoto kubwia kilaji
Mjadala huu nimeufuma kule kwa
mamanamwana.blogspot.com
nikaona ngoja na wadau wa globu ya jamii watie baraka zao...

-------------------------
Na Jiang Alipo
Mtoto huyu mkazi wa Dar es Salaam aliwashangaza wengi katika fukwe ya Coco Beach siku ya X Mas kwa umahiri wake wa kufakamia Safari Laga bila kutikisika. Kwa mujibu wa mama yake mdau huyu huondoka hadi bia mbili na yupo fiti.

Najua kitaalam hii haiko sawa kabisa lakini hii si mara ya kwanza kuona mtoto,tena wengine wadogo kuliko huyu, chini ya mwaka mmoja, akipewa pombe anywe. Wenyewe wanasema 'haina shida anaonja tuu'. Najua hata nyiyni wenzangu mmeshuhudia haya, na labda mnamjua mtoto angalau mmoja anayeonja.

Wazazi wenzangu mnasemaje juu ya tabia hii ya kuwaruhusu watoto kunywa vilevi wangali wadogo, hata kama ni kuonja tuu? na tufanyeje kuwashauri wazazi wenzetu wenye tabia hii waone adhari zake?
Picha na Mroki Mroki.

No comments: